info@wazohillsaccos.co.tz +255 764 472 730

Amana ya Mda Maalum

  • Service Type: Deposits
  • Date Created: 1 year ago

Amana ya Mda Maalum

Mwanachama akitaka kufunga akaunti hii, atapoteza sifa za kupata faida zilizozalishwa katika mwaka husika

Utaratibu wa akaunti hii, utakuwa kama ifuatavyo,

  • Mhusika atajaza fomu ya mkataba ya kufungua akaunti hiyo.
  • Akaunti hii haitozwi gharama za kufungua akaunti.
  • Kiwango cha chini cha kufungua akaunti hii ni Tsh 2,000,000/=
  • Mteja haruhusiwi kuchukua fedha kutoka akaunti hii hadi hapo mda wa mkataba utakapoisha
  • Riba zitakazolipwa kwenye akaunti ya amana maalum zitakuwa kama ifuatavyo.

Miezi 3

Miezi 6

Miezi 9

Miezi 12

5% p.a

7% p.a

8% p.a

11% p.a

 

  • Kiasi kitakachoanza kulipwa riba ni kuanzia Tshs. 2,000,000
  • Kama mwanachama ameamua kuvunja mkataba kwa kuchukua fedha kutoka akaunti hii kabla ya muda, itamlazimu kukosa faida ambayo angeipata katika kipindi hicho.
  • Mwanachama anayetaka kuchukua au kuongeza kiasi na muda katika akaunti ya Amana ya Muda Maalum atahitajika aonyeshe mkataba na stakabadhi iliyotumika wakati wa kuweka au kufungua akaunti.
  • Mwanachama aliyepoteza stakabadhi, atawajibika kuleta taarifa ya Polisi inayothibitisha upotevu huo; stakabadhi mpya itatolewa baada ya muda wasiku kumi na nne (14) za kazi na mhusika atawajibika kuchangia shs. 10,000/=.